Ooh Masikini, by Jamhuri Jazz Band
x2 |
Ooh Masikini
Mimi nina balaa sana
Tabu ni nyingi
Zinazonikaabili miye
Nitafanya nini ooh
Ulimwengu
Niwe na maisha
Kama wenzangu
Nitafanya nini ooh
Ulimwengu
Niwe na maisha
Kama wenzangu
|
x2 |
Nitafanya nini ooh
Maisha yananiendea vibaya miye
Kila ninalofanya miye ooh
Mauti yangu yangojewa kwa raha miye
Hakuna wema duniani ooh
Iliyobaki tumuombe Manani
Nitafanya nini ooh
Maisha yananiendea vibaya miye
Kila ninalofanya miye ooh
Mauti yangu yangojewa kwa raha miye
Hakuna wema duniani ooh
Iliyobaki tumuombe Manani
Tuwe Salama
Ooh tuwe salama
Ooh tuwe salama |
Wasiwasi Ondoa, by Jamhuri Jazz Band
x2 |
Ni nini Mama unalia ooo
Unalizwa nini ooo
Mimi ni wako wa zamani ooo
mwenzangu shaka ondoa
Ninapokuaga matata hayaishi nifanye nini sasa
Mwenzangu wanitafuta lawama mabaya mimi mwenzio
|
x4 |
Wasiwasi kwangu ondoa
jiepushe na majirani ooo
Mimi ni wako ooo
Wenzako wanaona wivu
Tunavyoishi mimi nawe
Mimi ni wako oo usife moyo |
Mganga N°1, by Jamhuri Jazz Band
x3 |
walinitesa sana ndugu zangu,
na kweli walifanikiwa,
na furaha walipata vijana,
kusikia mimi sisemi
|
|
wanyama wabaya maana yake,
sio simba wala si tembo,
ni wanadamu wenye choyo,
iyooo yalaaa
|
|
kaniki nilivalishwa,
hata chale nilichanjwa,
na madawa nilipakwa,
iyoo yalaa
|
|
mgonjwa amezidiwa,
haya mwite mganga,
haya shika mkoba,
iyoo iyoo iyoo
iyoo iyoo iyoo
iyoo iyoo iyoo
iyoo iyoo iyoo |
Simba Mwituni, by Jamhuri Jazz Band
x3 |
Aaee maria ee
Aaee maria ee
Bembeleza mwana oo
Msitu mkubwa oo
Safari ni ndefu tutaliwa na simba,
Oooo maria
Safari ni ndefu mama
Mwana analia ooo
Tutafanya nini ni mashaka sana
Oooo maria |
|